Klabu ya Simba imemaliza na mchezaji Said Ntibazonkiza na rasmi imemshukuru kwa muda
![](https://static.wixstatic.com/media/146e6d_d10cb46404e443d0a815cc70fc5c6647~mv2.jpg/v1/fill/w_147,h_147,al_c,q_80,usm_0.66_1.00_0.01,blur_2,enc_auto/146e6d_d10cb46404e443d0a815cc70fc5c6647~mv2.jpg)
wake aliotumikia klabu hiyo ambapo rasmi ameagwa.
Saido anaondoka Simba akiwa ameacha alama ikiwemo ya kuwa Top Scorer wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2022/23 na pia ndani ya Simba kwa msimu huu uliotamatika 2023/24.
"Uongozi wa klabu unautangazia umma kuwa hatutaendelea kuwa na mchezaji wetu Saido Ntibazonkiza baada ya mkataba wake kumalizika." Taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Instagram wa klabu ya Simba SC imeeleza.