Na VENANCE JOHN
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemchangia shilingi milioni tano Makamu Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA, Tundu Lissu ili kufanya matengenezo ya gari yake.
Katibu wa NEC, itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makala ndiye aliyeendesha harambee ya kumchangia Makamu Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu kiasi cha Shilingi Milioni 5.3 kwa ajili ya matengenezo ya Gari yake.
Harambee hiyo imefanyika jana, tarehe 14 Agosti 2024, kwenye Uwanja wa Furahisha, jijini Mwanza katika mkutano wa hadhara. Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema siasa si uadui hivyo ni vyema kushikana mkono pale inapobidi akisema wanasiasa wote wanalijenga taifa moja la Tanzania.
Comments