top of page

CHINA NI MSHIRIKA MUHIMU KWA UCHUMI WA ZANZIBAR: RAIS MWINYI

Na Ramla Ramadhan


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dk. Hussein Ally Mwinyi amesema kwa kipindi cha miaka mingi China imekuwa mshirika muhimu katika ukuaji wa uchumi Zanzibar kupitia sekta za uwekezaji na miradi ya ujenzi wa miundombinu


Ameyasema hayo katika mkutano wa mafunzo (warsha) maalumu wa kukuza uwekezaji, Biashara na Utalii uliofanyika katika ukumbi wa mkutano Waldorf Astoria jijini Shanghai ulioandaliwa na Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) kushirikiana na Ubalozi wa China, Tanzania


Mpaka sasa China ina jumla ya miradi 17 ya uwekezaji iliyosajiliwa Zanzibar yenye thamani ya takribani Dolla za Kimarekani Millioni 245 ambayo imetoa ajira za moja kwa moja kwa wananchi wa Zanzibar zipatazo 8,000


Pia China ni mshirika wa pili katika ukubwa kwenye Sekta ya Biashara Zanzibar ambapo thamani ya biashara katika Nchi hizo mbili imepanda kwa mwaka 2023 hadi kufikia Dola Millioni 66.5 na kukuza sekta ya Kilimo na viwanda


Mkutano huo ni hatua muhimu katika kuimarisha uhusiano baina ya Nchi hizo mbili katika maendeleo ya Nchi hususani uchumi na uwekezaji, kubadilishana fursa za biashara pamoja na teknolojia.

Commentaires


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page