top of page

DUA ZOTE ZIMEKATAA SASA AZAM FC KLABU BINGWA SIMBA SC SHIRIKISHO KULE KWA MTANI AZIZ KI TOP SCORER....

Hatimaye Ligi Kuu ya NBC imetamatika hii leo katika michezo 8 iliyopigwa kutoka kwenye viwanja tofauti tofauti hivyo kwa msimamo uliopo

Klabu ya Yanga SC ndio mabingwa huku washindi wa pili ni Azam FC na hawa ndio watashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika CAFCL.

Kwa upande wa nafasi ya tatu washindi ni Simba na nne ni Coastal Union ambapo hawa kwa



pamoja watacheza Kombe la Shirikisho Afrika CAFCC.

Aidha Play Off itakuwa ni kati ya JKT Tanzania na Tabora United FC kucheza play-off huku Geita Gold na Mtibwa wakishuka Daraja.

Aidha Mbio za Mfungaji Bora sasa zimefikia tamati huku Aziz Ki akiibuka Mfungaji bora kwa kuweka kambani mabao 21 ambapo mchezo huu wa mwisho ametupia mabao matatu (Hat- Trick) Yanga SC wakishinda 4 - 1 dhidi ya Prisons ambapo amemtupa chini Feisal Salum aliyemaliza msimu kwa mabao 19 akifunga bao moja kwenye mchezo wa leo dhidi ya Geita Gold uliotamatika kwa 0 - 2.

Simba SC 2-0 JKT Tanzania

Coastal Union 0-0 KMC

Mashujaa FC 3-0 Dodoma Jiji

Ihefu SC 5-1 Mtibwa Sugar

Yanga SC 4-1 Prisons

Namungo FC 3-2Tabora United

Geita Gold 0-2 Azam FC

Singida FG 2-3 Kagera Sugar

Asante kwa kufatilia ukurasa wako wa Msasa Media hususani kwenye upande wa habari za michezo kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 tukutane msimu ujao wa 2024/25 panapo majaliwa.



Kommentare


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page