Katibu wa Baraza la Mawaziri Jumuiya ya Afrika Mashariki Peninah Malonza amethibitisha kuwa majadiliano kati ya Ethiopia na wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC yanaendelea vizuri na yako katika hatua ya mwisho kwa ajili ya nchi hiyo kuwa nchi
mwanachama mpya wa Jumuiya hiyo. Iwapo Ethiopia itajiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, itakuwa nchi ya 9 kuunganisha jumuiya hii ambayo inaundwa na nchi za Tanzania, Burundi, DRCongo, Rwanda, Kenya, Uganda, Sudan Kusini na Somalia.
Kukaribia kwa Ethiopia kujiunga na EAC kunaashiria hatua nyingine katika kuimarisha uhusiano wa kikanda na kukuza maendeleo ya pamoja.
Kujiunga kwa Ethiopia ambayo ipo katika hatua za mwisho kuwa nchi mwanachama mpya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), itaongeza idadi ya watu ndani ya kanda hiyo hadi kufikia watu milioni 420.
コメント