top of page

FACEBOOK KUANZA KUWALIPA WAZALISHA MAUDHUI NCHINI TANZANIA

Na VENANCE JOHN


Kampuni ya META inayomiliki mitandao ya Facebook na Instagram imesema Watengeneza Maudhui nchini Tanzanja wanaotumia mitandao hiyo wataanza kulipwa kuanzia mwezi huu (Agosti 2024) ikiwa ni baada ya kukamilika kwa mazungumzo kati yake na Serikali ya Tanzania.


Pia, META imelishukuru jukwaa la JamiiForums kwani ndiyo waliofanikisha mazungumzo kati META na Mamlaka za kiserikali pamoja na juhudi za kuhakikisha wazalishaji wa maudhui wanaelewa na kufuata Sera na mazingira salama na endelevu ya mtandaoni


Ikumbukwe kuwa, Machi 9, 2024, JamiiForums iliandaa mkutano na wabunifu wa maudhui mtandaoni (Wanawake) ili kujadili changamoto wanazo kutananazo kwenye majukwaa ya kidijitali ikiwemo masuala ya malipo.


Credits: JamiiForums

留言


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page