Ni usiku wa Admin na Mpiga picha wa klabu kubwa ya Soka nchini Tanzania @rabbihume ambaye ameaga uakapera kwa kufunga ndoa na mwanadada @peace_perry na usiku wa leo
rasmi wanasherehekea harusi yao.
Mpiga picha huyu ambaye amekuwa akifanya vyema kwa miaka mingi amejizolea wapenzi wengi kutokana na uhodari wa kupiga picha kali na zenye mvuto ikiwemo ile ya bao la Sakho ambalo lilimpa tuzo ya bao bora CAF.
Sherehe hiyo inaongozwa na Mshereheshaji maarufu nchini Tanzania MC Garab na inahudhuriwa na watu mbalimbali mashuhuri wakiwemo wachezaji ambapo hadi hivi sasa tayari Captain wa klabu hiyo kwa sasa @official_mohamedhussein15 ameshawasili.
Comments