top of page

JAHAZI YA CLOUDS FM SASA NI CHINI YA GEORGE BANTU, B DOZEN NA ADAM MCHOMVU.

Mkuu wa Maudhui wa Clouds Media Group Sebastian Maganga leo kupitia Power Breakfast ya Clouds FM ameutaja urithi wa Marehemu Gadner G. Habash kwenye kipindi chake cha Jahazi alichokua akikifanya kwa miaka mingi kabla ya kufariki mwezi April 2024.




Urithi huo ni Watangazaji wataoliendesha JAHAZI ambapo amewataja kuwa ni Mwenyeji George Bantu, Hamisi Mandi (BDozen), Adam Mchomvu na DJ D Ommy huku Watayarishaji (Producers) wakiwa ni Musa Memba na Big Chawa.

Ikumbukwe kuwa kwa miaka mingi B Dozen na Mchomvu walikuwa wakitangaza kipindi cha mchana cha burudani Double XXL wakiwa na Kennedy The Remedy, Meena Ally pamoja na John Jackson.


Comments


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page