![](https://static.wixstatic.com/media/146e6d_5775710169344f8ab1b7612b6142f697~mv2.jpg/v1/fill/w_147,h_147,al_c,q_80,usm_0.66_1.00_0.01,blur_2,enc_auto/146e6d_5775710169344f8ab1b7612b6142f697~mv2.jpg)
Klabu ya Simba SC imemuongezea mkataba wa mwaka mmoja mchezaji wake Kibu Denis na sasa atakuwa kwenye viunga vya wana Msimbazi hadi mwaka 2026.
Simba inampa mkataba huu Kibu wakati ikiendelea kufyeka baadhi ya wachezaji ambapo miongoni mwa waliokwisha kupewa Thank You ni pamoja na Inonga Baka, Luis Miquissone, Kennedy Juma, Shaban Chilunda, Saido Ntibazonkiza na Bocco.