top of page

KILA KITU KINGEKUWA SAWA TUNGESHINDA - AHMED ALLY

Hatimaye Meneja habari na mawasiliano Simba SC Ahmed Ally ameibuka na kuzungumza juu ya mchezo wa jana dhidi ya Yanga SC waliopoteza kwa kufungwa bao moja sifuri kwenye Ligi Kuu ya NBC ambapo ameandika ujumbe huu kupitia ukurasa wake wa Instagram. "Tunaumia kwa kupoteza mchezo wa derby lakini tunajipongeza kwa kuwa mradi wetu wa kutengeneza timu umeanza kutoa matunda tena kwa haraka sana


Wote ni mashahidi misimu kadhaa nyuma tulifungwa derby na kutawalia na mpinzani kwa dakika zote 90. Jana tumeona tofauti kubwa sana tumefungwa lakini tumeutawala mchezo kwa asilimia kubwa na kama kila kitu kingekua sawa basi tungeshinda mchezo ule


Muhimu kwetu Wana Simba kwanza tukubali tumepoteza na wala hakuja haja ya kuanza kuhesabu tumepoteza mara ngapi, Mpira ni maisha ya duara muda wetu utafika na sisi tutatawala derby kwani tumewahi kufanya hivyo


Muhimu kwa sasa ni kusahau yote yaliyotokea na kujipanga upya kwa vita iliyo mbele yetu. Tumebakiwa na michezo 24 nguvu kubwa iwe kushinda michezo hiyo tumepoteza derby sio ubingwa Na pia tuwekeze nguvu kwenye mchezo wetu Jumanne dhidi ya Tanzania Prison

Ubaya Ubwela unaendelea."

Comments


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page