Hatimaye Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Ally amethibitisha kuandama kwa mwezi leo April 09,2024 ambapo amesema kesho April 10,2024 ni Sikukuu ya Eid Al Fitr. "Leo April 09,2024 nimepokea taarifa za mwezi kuandama kutoka Mombasa na Lamu Kenya na pia Pemba Visiwani Zanzibar na Ofisi ya Mufti Zanzibar imethibitisha, hivyo Mimi kama Mufti wa Tanzania nathibitisha kuandamana kwa mwezi na kesho April 10,2024 itakuwa ni Eid Al Fitr niwatakie Eid njema"
top of page
Radio on air
Msasa Media
Follow, like, comment, and share
Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam
bottom of page
Commentaires