Miezi miwili Msasa Online tulikupasha juu ya taarifa ya Mwanaume mwenye umri wa miaka 62
aliyetambulika kwa jina la Richard Slayman ambaye alikuwa binadamu wa kwanza kupandikizwa Figo ya Nguruwe, sasa taarifa tulizozipokea dawati la habari ni kwamba mwanaume huyu amefariki dunia siku ya jana.
Richard amefariki dunia baada ya kukaa na figo hiyo kwa muda wa miezi miwili.
Ikumbukwe kuwa zoezi hilo la kupandikizwa Figo ya Nguruwe lilifanyika kwenye Hospitali ya General Hospital huko Massachusetts nchini Marekani Marekani.
Comments