Klabu ya Simba SC imemuongezea mkataba wa mwaka mmoja mchezaji wake Mzamiru Yasin na sasa atakuwa kwenye viunga vya wana Msimbazi hadi mwaka 2026.
Simba inampa mkataba huu Mzamiri wakati ikiendelea kufyeka baadhi ya wachezaji ambapo miongoni mwa waliokwisha kupewa Thank You ni pamoja na Kennedy Juma, Chilunda, Saido Ntibazonkiza na Bocco.