POGBA AFUNGIWA MIAKA MINNE...
Kiungo wa Klabu ya Juventus na timu ya Taifa ya Ufaransa Paul Pogba amepigwa marufuku
kucheza soka kwa miaka minne na Mahakama ya kupambana na dawa za kulevya nchini Italia.
Hukumu hiyo inaweza kumaliza safari ya soka ya Pogba, kwani mwezi ujao, atatimiza miaka 31
Pogba alirejea Juventus kutoka Manchester United mnamo 2022 lakini alikabiliwa na majeraha, akicheza mechi 6 pekee Serie A, Juventus msimu uliopita na mbili msimu huu.
Comments