Na VENANCE JOHN
Rais wa Urusi Vladimir Putin leo amezishutumu nchi za Magharibi kwa kuisukuma Urusi kwenye kile alichokiita mistari nyekundu hali ambayo imeweka wazi hadharani kuwa haitaivumilia na kusema Urusi inalazimishwa kujibu.

Putin aliuambia mkutano wa maafisa wa ulinzi kuwa Urusi inatazama mienendo ya Marekani na uwezekano wa kupeleka makombora ya masafa mafupi na ya masafa ya kati kwa ajili ya kukabiliana na hali.
Amesema Urusi itaondoa vizuizi vyake vyote vya na kupeleka makombora yake ikiwa kwa ajili ya kuanza kutumika kama Marekani itaendelea na kusambaza makombora ya ATACMS kwa Ukraine. Putin, ambaye amesema vikosi vya Urusi nchini Ukraine vimechukua udhibiti wa makaazi 189 hadi sasa mwaka huu, amesema silaha za nyuklia za Urusi ziko kwa ajili ya kutumika.
Comments