top of page

RAIS WA KWANZA WA NAMIBIA SAM NUJOMA AFARIKI DUNIA

Taarifa zilizotufikia mezani Rais wa Kwanza wa nchi ya Namibia, Sam Nujoma amefariki Dunia akiwa na umri wa Miaka 95.


Sam Nujoma aliongoza mapambano ya kupigania Uhuru wa nchi hiyo kutoka kwa utawala wa Afrika Kusini Mwaka 1990 ilipopata Uhuru. Moja ya matukio yake ya kukumbukwa ni Mwaka 1960 alipokimbilia Nchini Tanzania kutokana na vuguvugu lililotokea Namibia, ambapo Hayati Mwalimu, Julius alimpatia hifadhi


Baada ya Uhuru alichaguliwa kuwa Rais na kudumu hadi Mwaka 2005 ambapo aliamua kustaafu ila alibaki kuongoza Chama cha South West Africa People's Organisation (SWAPO) hadi Mwaka 2007.

Comentarios


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page