![](https://static.wixstatic.com/media/146e6d_56af032164064198a1c26d18012189eb~mv2.jpg/v1/fill/w_147,h_147,al_c,q_80,usm_0.66_1.00_0.01,blur_2,enc_auto/146e6d_56af032164064198a1c26d18012189eb~mv2.jpg)
Rais wa Klabu ya Yanga SC Eng. Hersi Said amemkabidhi zawadi ya jezi ya Yanga SC mchezaji Achraf Hakimi anayekipiga kunako klabu ya PSG ya nchini Ufaransa.
Hakimi ambaye ni raia wa Morocco yupo nchini Tanzania kwa mapumziko kipindi hiki cha likizo ambapo ligi mbalimbali duniani zimemalizika, Hakimi ametembelea vivutio kadhaa vya utalii ikiwemo Hifadhi za Taifa za Serengeti na Ngorongoro.