Hatimaye mchezaji Edward Manyama ameaga rasmi kunako klabu ya Azam FC tayari kwa
kwenda kutafuta changamoto sehemu nyingine ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram amefunguka haya "Bye bye Azam FC bye bye Chamazi ni ngumu sana ila ni wakati sahihi wa mimi kuondoka kwenye familia ya Azam FC nimeshindwa hata kuandika kwa sababu ya upendo wenu (wafanyakazi) (wachezaji) (benchi la ufundi) (viongozi) (mashabiki) nawatakia maisha yenye furaha na malengo tele Mungu awabariki sana sana".
Comments