Kutoka nchini Sudan Kusini Serikali imeamuru kufungwa kwa muda usiojulikana kwa Shule zote kutokana na joto kali ambalo linatarajiwa kufikia hadi nyuzi joto 45 (113F) na kudumu kwa
wiki mbili, huku ikionya kuwa Shule ambayo itakaidi maagizo hayo itafutiwa usajili wake
Nchi hiyo inapitia Vipindi virefu vya Joto wakati wa mchana na usiku ambapo Mamlaka za Afya na Elimu pia zilihimiza Wazazi kuzuia Watoto wao kucheza nje kwa muda mrefu
Imeripotiwa kuwa katika Juma lililopita pekee Watoto 15 wamefariki kwa Homa ya Uti wa Mgongo na Joto Kali.
Comments