SIMBA SC WAACHANE NA CHAMA - WILSON ORUMA
Mchambuzi wa soka Wilson Oruma amesema
"Simba wakimuongezea mkataba Chama hatawasaidia kama muda huu ambao anaonekana kuna kitu anakitafuta (mkataba mpya), Simba wanatakiwa kufanya maaamuzi magumu ya kumuambia Chama THANK YOU, kuna muda unatakiwa kukiacha unachokipenda ili upate unachokitaka,"
"Kwa sasa Chama anafanya vizuri kwa kuwa kuna kitu anakitaka lakini akishakipata atarudi kule kule yaani Chama kama Pogba akiwa anataka jambo lake anakupa kitu extra tofauti na akishakipata huwa anabweteka, Mimi naona muda wa Chama kuitumikia Simba umeshaisha hivyo wanatakiwa kuachana naye kwani naamini Chama hana cha ziada kuisaidia Simba".
Comments