Na VENANCE JOHN
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuundwa kwa kikosi kazi kinacholenga kutokomeza kile alichokiita chuki dhidi ya Wakristo ndani ya serikali ya Marekani. Trump ametoa tangazo hilo jana mjini Washington, DC, katika hafla ya kila mwaka ambayo huleta pamoja vikundi vya kidini na viongozi wa serikali.
![](https://static.wixstatic.com/media/57c8da_c4319a6607d64a6ea456ea35265a79d6~mv2.jpeg/v1/fill/w_980,h_980,al_c,q_85,usm_0.66_1.00_0.01,enc_avif,quality_auto/57c8da_c4319a6607d64a6ea456ea35265a79d6~mv2.jpeg)
Wakati wa hotuba yake, Trump amesema kwamba atatia saini amri ya utendaji na kumteua Mwanasheria Mkuu wa Marekani Pam Bondi kuongoza juhudi hizo. Pia ametaja mashirika kadhaa ya serikali ambayo yanaweza kuchunguzwa chini ya juhudi, ikiwa ni pamoja na Idara ya Haki (DOJ) na Huduma ya Ndani ya Mapato (IRS).
"Dhamira ya kikosi kazi hiki itakuwa kushikilia mara moja aina zote za ulengaji na ubaguzi dhidi ya Ukristo ndani ya serikali ya shirikisho, pamoja na idara ya haki (DOJ), ambayo ilikuwa mbaya kabisa, huduma ya mapato (IRS), shirika la ujajusi (FBI) na mashirika mengine," Trump amesema.
Chini ya Katiba ya Marekani, serikali inalinda uhuru wa dini lakini baadhi ya watetezi wa uinjilisti wamedai kuwa Ukristo ni sehemu ya msingi ya mfumo wa serikali ya Marekani kwani Trump alikuwa akilipenda kundi hilo katika kampeni zake zote za kuwania urais.
Comentários