top of page

TUMBILI WASABABISHA UMEME KUKATIKA NCHI NZIMA SRI LANKA

Na VENANCE JOHN


Waziri wa nishati nchini Sri Lanka, Kumara Jayakody amelaumu tumbili kwa kusababisha kukatika kwa umeme kote nchini humo kwa madai kuwa aliingia kwenye kituo cha uzalishaji umeme kusini mwa mji mkuu wa Colombo.


Umeme umeshaanza kurejeshwa taratibu katika taifa hilo lenye watu milioni 22, huku vituo hosipitali na mitambo ya kusafisha maji vikipewa kipaumbele. "Tumbili aligusa transfoma ya gridi yetu, na kusababisha kukosekana kwa usawa katika mfumo wa umeme," Waziri wa Nishati Kumara Jayakody amewaambia waandishi habari.

Comments


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page