top of page

TUMEIBA KIUNGO WAO AIRPORT NI ZAIDI YA AUCHO NGOJENI DERBY IFIKE MUONE - ALLY KAMWE

Kutoka kwa Afisa Habari wa Yanga SC Ally Kamwe amepost picha hii kisha amefunguka haya

Utapeli wa aina 10 wa Viongozi wa KOLO kwa Mashabiki wao

1: Mimi nina uzoefu, Mkinichagua niwe kiongozi Yanga hawezi kutufunga, Viongozi wao vijana wale hawaniambii chochote. [ Sasa hivi ameanza kukimbia kuja uwanjani]

2: Kolo hafungwi na Yanga mvua ikiwa inayesha [5-1 ikazaliwa]

3:: Kolo akiweka kambi Zanzibar, Yanga hachomoki, Twendeni huko Tukajifungie [2-1 Swaafi wakachezea]

4: Kolo ikiunga nguvu na Friends Of Kolo washirikishwe, Yanga anakufa asubuhi tu [Vikao mpaka wametumia Calculator lakini wapi

5: Kolo ni kubwa sana, Haiwezi kufungwa mara mbili ndani ya Msimu mmoja [ Jumla ya Goli 7 zimepatikana Nje, Ndani]

6: Yanga hawezi kufikia mafanikio yetu Kimataifa, watatamba hapa hapa tu [Medali ya Shirikisho CAF iko Jangwani, Robo Fainali CAF CL

7: Sisi Kolo tuweke nguvu Kimataifa, Tutampasua Al Ahly na kumtoa [Wakaishia kutoa picha za Mayele tu

8: Kolo Tumeshusha mastraika wakuwatawanya bahari, watawafunga magoli ya kila aina. Ni funga funga hao [Derby wote wamekaa benchi wakikata kucha kwa meno

9: Aaah Kibu Dee ndio mechi zake, Diarra atakoma. Huyu ndio kiboko ya Yanga [Mechi 2 kwenye Derby hana On Target hata 1



10: Tumeiba kiungo wao Airport, huyu ni zaidi ya Aucho, Anajua sana, Ngojeni Derby ifike muone anavyobadilika na kuwa hatari [Alichoweza kubadili ni rangi ya Nywele Tu

Nb: Kwa sauti ya GSM "YANGA BINGWA" Ameandika Ally Kamwe.

Comments


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page