Baada ya kuwa kimya kwa karibu siku mbili toka timu yake ipoteze kwa mtani Yanga 2 - 1
Meneja habari na mawasiliano Simba SC Ahmed Ally ameibuka na kuchapisha ujumbe huu kupitia ukurasa wake wa Instagram
"Dhahabu hupitishwa kwenye moto mkali ili ipate thamani na iwe bora
Licha ya kuwa huteseka inapopita kwenye moto huo lakini mwishoe hubaki safi, bora na thamani yake huongezeka maradufu
Wana Simba tuvumilie kupita kwenye moto huu mkali ili tuwe bora na hadhi yetu irejee
Najua maumivu ni makubwa kwa kua moto mkali lakini hatuna budi kuvumilia kwani ndio njia pekee ya kurudi kwenye thamani yetu.
Tutafurahi tu muda wetu umekaribia
This time soon."
Comments