top of page
Radio on air

UHISPANIA, NORWAY NA IRELAND ZALITAMBUA RASMI TAIFA LA PALESTINA...

Waziri Mkuu wa Uhispania anaita serikali ya Palestina 'njia pekee ya amani'; Israel inaishutumu Madrid kwa uchochezi kwa Wayahudi 'mauaji ya halaiki'.

Kuanzishwa kwa taifa la Palestina ndiyo "njia pekee ya amani" katika Mashariki ya Kati, Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez amesema wakati nchi yake ikitangaza kutambuliwa rasmi kwa taifa hilo, pamoja na Norway na Ireland.

Sanchez alizungumza Jumanne kabla ya baraza la mawaziri kupiga kura iliyoidhinisha mpango uliotangazwa hapo awali wa kutambua taifa la Palestina.

Utambuzi wa Norway pia umeanza kutekelezwa, huku Ireland nayo ikifuata mkondo huo.




Msemaji wa serikali ya Uhispania Pilar Alegria alitangaza kwamba baraza la mawaziri "limepitisha uamuzi muhimu wa kutambua taifa la Palestina", ambao ulikuwa na "lengo moja: kusaidia Waisraeli na Wapalestina kupata amani".

Waziri mkuu wa Uhispania aliita hatua hiyo "suala la haki ya kihistoria."

"Njia pekee ya kufikia amani ni kuanzishwa kwa taifa la Palestina, kuishi bega kwa bega na taifa la Israel," alisema.

"Mamlaka ya Palestina lazima lijumuishe na Ukingo wa Magharibi na Gaza zilizounganishwa na ukanda na Eastern Jerusalem kama mji mkuu wake."

Madrid haitatambua mabadiliko yoyote kwenye mipaka ya kabla ya 1967 isipokuwa kama itakubaliwa na pande zote mbili, alisema.

Ukingo wa magharibi wa Mto Jordan, Eastern Jerusalem na Ukanda wa Gaza ulikuwa sehemu ya eneo lililotnyakuliwa na Israeli mnamo 1967 katika Vita ya Israel Arab War.

Viongozi wa Uhispania, Ireland, Malta na Slovenia walisema mwezi Machi kwamba walikuwa kwenye hatua za kutambua taifa la Palestina kama "mchango chanya" katika kumaliza vita huko Gaza.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway Espen Barth Eide alisema katika taarifa yake, "Kwa zaidi ya miaka 30, Norway imekuwa mojawapo ya watetezi wenye nguvu wa taifa la Palestina. Leo, wakati Norway inaitambua rasmi Palestina kama taifa, ni hatua muhimu katika uhusiano kati ya Norway na Palestina.

Baraza la mawaziri la Ireland liliidhinisha kutambuliwa rasmi muda mfupi baada ya bendera ya Palestina kupandishwa huko Dublin nje ya makao ya bunge la Ireland.

"Huu ni wakati muhimu na nadhani unatuma ishara kwa ulimwengu kwamba kuna hatua za kivitendo ambazo unaweza kuchukua kama nchi kusaidia kuweka matumaini na hatima ya suluhisho la serikali mbili hai wakati ambapo wengine wanapitia kipind kigumu na huzuni...” Waziri Mkuu wa Ireland Simon Harris alisema.

Malta na Slovenia zimependekeza pia zitachukua hatua sawa, ingawa sio mara moja.

Harris alimtaka Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu "kusikiliza ulimwengu na kuacha janga la kibinadamu tunaloona huko Gaza."

Hata hivyo, matangazo hayo yalizua ghadhabu tu kutoka kwa Israel, na kuongeza kutoelewana kwake na baadhi ya mataifa ya Umoja wa Ulaya kuhusu kuendelea kwa vita huko Gaza.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Israel Katz alimshutumu Sanchez wa Uhispania kwa kuwa "mshirika mchochezi" wa "mauaji ya kimbari" ya Kiyahudi.

Akitoa maoni yake.

Hispania, Ireland na Norway zilitangaza mpango wao wa kuitambua rasmi Palestina wiki iliyopita, na kuifanya Israel kuwaita tena mabalozi wake kutoka nchi zote tatu.

Palestina tayari imetambuliwa na nchi nyingine 144.

Kati ya wanachama 27 wa EU, Uswisi,Hungary, Jamhuri ya Czech, Poland, Slovakia, Romania na Bulgaria wametambua taifa la Palestina.

Uingereza na Australia zimesema zinazingatia kutambuliwa kwa Palestina, Ufaransa imesema sasa si wakati ambapo Ujerumani iliungana na mshirika mkuu wa Israel, Marekani, kukataa mtazamo wa upande mmoja, na kusisitiza kuwa suluhu ya serikali mbili inaweza kupatikana tu kwa njia ya mazungumzo.

Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page