.....Kundi la waasi la wahuthi wa Yemeni wamedai kuwa wakiwa na dola la IS la nchini Iraq wameshambulia maeneo muhimu ya taifa la Israeli.
![](https://static.wixstatic.com/media/146e6d_76e1ed0c8a80409b80b4532dfa6879bf~mv2.jpg/v1/fill/w_147,h_147,al_c,q_80,usm_0.66_1.00_0.01,blur_2,enc_auto/146e6d_76e1ed0c8a80409b80b4532dfa6879bf~mv2.jpg)
Oparesheni ya kijeshi imefanyika, msemaji wa Huthi Yahya Saeed amesema katika hotuba iliyorushwa na runinga bila hata hivyo kuyataja maeneo hasa yaliyolegwa na kushambuliwa
Kundi la wahuthi limekuwa likianzisha mashambulizi ya makombora kwa ndege zisizokuwa na rubani maarufu kama drone tangu mwezi novemba mwaka jana kwa kile kundi hilo linachosema ni mshikamano kwa Wapalestina katika vita inayoendelea katika ukanda wa Gaza.
Mpaka sasa tayari kundi la huthi limeshazamisha meli mbili, kuteka meli moja na kuwaua mabaharia watatu.