top of page

WANASIMBA TUTULIE TUWAPE MUDA VIONGOZI WETU WATAFUTE KOCHA MWINGINE MZURI - AHMED

Kutoka kwenye ukurasa wa Meneja habari na mawasiliano Simba SC Ahmed Ally amefunguka haya baada ya Klabu yake kuachana na kocha wao Benchikha

"Moja kati ya Kocha bora kuwahi kuwa nao Simba Sports




Haikua rahisi kumpata Mwalimu wa kaliba yake na hakuna aliyeamini kama tungemudu kuwa na kocha wa aina hiyo

Kumpata Mwalimu huyu ni ishara kuwa viongozi wetu walionesha dhamira ya dhati ya kuipeleka Simba kwenye kilele cha mafaniko makubwa zaidi

Ukubwa wa Mwalimu Benchikha na gharama za kuwa na Mwalimu wa aina yake ni dhahiri kuwa viongozi wetu wakiongozwa na @moodewji walijitoa mhanga kwa maslahi ya kuiboresha Simba yetu Juhudi ya kwanza ilikua ni kumleta Kocha jambo ambalo limefanyika kwa asilimia mia juhudi ya pili ilikua ni kubaki nae Kocha kubaki kazini au Muajiriwa yeyote kubaki kazini hutegemea pia na matakwa ya muajiriwa binafsi Wana Simba tutulie tuwape muda viongozi wetu watafute Kocha mwingine mzuri kwa maslahi ya timu, Kama waliweza kumleta Benchikha basi wanaweza kuleta yeyote mzuri kwa maslahi ya Simba yetu

Maisha yanaendelea!!". Ahmed Ally.

Comentarios


Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page