top of page

WANAWAKE TUSAIDIENI KUTULEA - MHE. PINDA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi mhe. Geophrey Mizengo Pinda (Mb.) amewataka wanawake wote nchini kushikama katika kuilea jamii ya watanzania ili kujenga jamii iliyo staarabika katika nyanja zote za maendeleo endelevu ya Taifa.


Mhe. Pinda amesema hayo tarehe 21 Desemba 2024 katika alipokuwa mgeni rasmi hafla ya uzinduzi wa kitabu cha NGUVU YA MALENGO iliyofanyika katika ukumbi wa Cavillan Social Hall Jijini Dodoma.

"Wamama mimi niendelee kuwapongeza msirudi nyuma mnatulisha familia zetu zinaishi kwa migongo yenu nyingi sana" amesema Naibu Waziri Mhe.Pinda "Kwa hiyo ni wapongezee wamama, wamama kaza kamba tusaidieni tuleeni" ameongeza Mhe. Pinda


Aidha mhe. Pinda amewataka watanzania kote nchini kuunga jitihada za maendeleo za Serikali ya awamu ya sita iliyoko chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan. "Mama Samia ni nguvu ya malengo ya nchi yetu kwa sababu alichokilenga anataka kifike na aone matokea yake" amesema Naibu Waziri mhe. Pinda


Ameongeza kuwa dhamira ya dhati ya Rais Samia ya kuwaletea wananchi Maendeleo imeleta mabadiliko makubwa ndani na nje ya nchi kwa kuendeleza miradi ya kimkakati ya watangulizi wake katika awamu zilizopita.

Comments

Couldn’t Load Comments
It looks like there was a technical problem. Try reconnecting or refreshing the page.
Msasa Media
  • Instagram
  • Facebook
  • X
  • Youtube
  • TikTok

Follow, like, comment, and share

Tel. +255758379300
Mbezi Dar es saalam

bottom of page