Na mwandishi wetu Venance John
Umoja wa mataifa umesema wapalestina milioni 2.5 Kusini mwa Gaza wameathiriwa na
![](https://static.wixstatic.com/media/146e6d_79ad13b55e6a4d668856fe4a052dcfab~mv2.jpg/v1/fill/w_147,h_147,al_c,q_80,usm_0.66_1.00_0.01,blur_2,enc_auto/146e6d_79ad13b55e6a4d668856fe4a052dcfab~mv2.jpg)
tangazo lililotolewa na jeshi la Israeli likiwataka kuhama eneo hilo.
Watu wengi wamekuwa wakiingia eneo la Khan Younis kwa mguu na kwa magari wakitoka maeneo mbalimbali kukimbia mapigano kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wanamgambo wa Hamas
Wagonjwa na wafanyakazi wa wameanza pia kuikimbia hospitali kubwa katika eneo hilo ingawa jeshi la Israel limesema hawakuwa welengwa wa amri ya kuhama
Maafisa wa afya wa Gaza wanasema Wapalestina nane wameuawa na dozeni ya wengine kujeruhiwa katika mashambulizi ya usiku wa kuamkia siku ya jumanne
Louise Wateridge afisa wa shirika la misaada la Umoja wa Mataifa linalowashughulikia wakimbizi wa Wapalestina UNRWA amewaomba watu waondoke kwa kuwa wamelazimika kuyaacha tena makazi yao.