Huu ni muendelezo wa taarifa tuliyokupasha siku chache zilizopita juu ya mwanadada aliyebakwa mbele ya mumewe.
Sasa Polisi nchini India wamewakamata watu nane kuhusiana na shambulio na ubakaji wa
genge la wanablogu wawili wa Uhispania wanaotumia pikipiki kusafiri maeneo mbalimbali (Mke na Mume) mwishoni mwa wiki iliyopita katika jimbo la Jharkhand mashariki.
Polisi walisema waliwapata wawili hao ambao ni mume na mke siku ya Ijumaa jioni katika wilaya ya Dumka jimbo ambapo wanandoa hao walikuwa wamepiga kambi. Polisi walisema wawili hao walionekana kana kwamba walikuwa wamevamiwa. Walipopelekwa katika hospitali ya eneo hilo, mke alimwambia daktari kwamba alibakwa.
Awali watu watatu walikamatwa Jumamosi, na, katika mkutano na wanahabari Jumatatu, polisi walitangaza kuwa wamewakamata wanaume wengine watano kuhusiana na tukio hilo.
Comments