Taarifa kutoka nchini Kenya Waziri wa Utalii nchini humo Alfred Mutua akiwa amemtembelea na kumjulia hali Ofisa wa Polisi, David Maina ambaye alipoteza viganja vya mikono yote miwili
baada ya kitoa machozi kulipuka wakati wa maandamano yanayoendelea nchini humo.Mutua amemtembelea ofisa huyo leo Juni 20, 2024 katika Hospitali ya Nairobi West ambako anaendelea kupata matibabu baada ya kupata majeraha hayo juzi Jumanne wakati wa maandamano.
Maandamano hayo ambayo yameingia siku ya tatu leo ambapo wananchi wanapinga mapendekezo ya kuongeza kodi katika Muswada wa Fedha wa 2024 ambao uliwasilishwa bungeni Juni 18, mwaka huu.
Source: Mwananchi