Kutoka nchini Msumbiji taarifa zilizotufikia asubuhi hii zinaeleza kuwa zaidi ya Watu 90 wameripotiwa kufariki katika ajali ya Kivuko kinachodaiwa kilikuwa na takriban Watu 130 katika eneo la jirani na jimbo la Nampula, huku Watu 5 wakiokolewa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na uongozi wa eneo hilo, imeelezwa kuwa miongoni mwa waliopoteza maisha ni Watoto na chanzo cha ajali ni uzito kuzidi kwenye Kivuko.
Comments